Drogba akiwa katika uzi wa Ivory Coast. |
MFUKO wa Didier Drogba, leo utafanya hafla ya uchangishaji
fedha katika hoteli ya Dorchester Hotel mjini London, lengo likiwa ni kukusanya
kiasi cha pauni Milioni 3 kwa ajili ya mradui wa ujenzi wa hospitali nchini
kwao Ivory Coast.
Zoezi hilo la tatu kufanyika katikia mradi huo, linatarajiwa
kuhusisha watru kibao maarufu, wakiwemo wanasoka nyota duniani na wanasiasa, alisema
mshambuliaji wa Chelsea.
Mazagazaga kibao, zikiwemo jezi za mchezaji huyo, rafiki
zake na wachezaji wenzake, viatu, soksi na kadhalika vitauzwa kwenye zoezi hilo
la hisani.
“Sapoti ambayo foundation yangu imepata hadi sasa ni babu
kubwa, lakini bado tuna kazi zaidi ya kufanya,” alisema Nahodha huyo wa Ivory Coast.
Kituo cha afya cha Gigantic kinajengwa katika wilaya ya
Attecoube mjini Abidjan, eneo la watu fukara ambalo linakosa hadi zana za
kisasa za tiba.
Drogba alisema tiba na huduma kwa ujumla katika hospitali
hilo, zitakuwa zikitolewa bure.
Mfuko huo (Didier Drogba Foundation) ulianzishwa mwaka 2007,
kwa lengo la kushughulika na masuala ya kiafya na elimu Afrika.
0 comments:
Post a Comment