// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); DROGBA ACHANGISHA PAUNI MILIONI 1.2 - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE DROGBA ACHANGISHA PAUNI MILIONI 1.2 - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Wednesday, March 14, 2012

    DROGBA ACHANGISHA PAUNI MILIONI 1.2


    Drogba
    MSHAMBULIAJI wa Chelsea, Didier Drogba Jumamosi ya Machi 10 alichangisha kiasi cha Pauni Milioni 1.2 kupitia mfuko wake wa hisani, katika shughuli iliyofanyika kwenye hoteli ya Dorchester mjini London.
    Fedha hizo zinafanya jumla ya Pauni Milioni 3 zilizochangishwa na mfuko wake kwa ajili ya ujenzi wa hospitali nchini mwao, Ivory Coast.
    Tukio hilo lilivutia watu kibao maarufu kuanzia wanasoka nyota duniani, waburidishaji, wanasiasa na nyota wa Chelsea, John Terry, Frank Lampard, Ashley Cole, Michael Essien, Petr Cech, Branislav Ivanovic, Florent Malouda, Salomon Kalou, Paulo Ferreira, Ross Turnbull na Hilario waliohudhuria kumsapoti mchezaji mwenzao.
    Wachezaji wa Arsenal, Bakary Sagna na Gervinho sambamba na Emmanuel Adebayor wa Tottenham nao walihudhuria.
    Kiasi kizuri cha mchango kilitoka kwa watu binafsi, wakati kiasi cha pauni 240,000 kilitokana na mauzo ya jezi, viatu, soksi, headbands na bidhaa nyingine.
    Rapa Muingereza, Wretch 32 alijishindia saa ya dhahabu baada ya kutoa mchango mkubwa.
    Drogba aliwashukuru wageni wake kwa kusema: “Sapoti ambayo mmeonyesha kwa foundation yangu hadi sasa ni kubwa sana. Nina furaha uko hapa na umechangia kufanikisha ujenzi wa hospitali hii.”
    Kituo cha afya chja Gigantic kitajengwa wilaya ya Attecoube mjini Abidjan, eneo la watu masikini linalokosa vifaa vya kisasa vya huduma za afya.
    Drogba alisema ushauri na matibabu vitakuwa vikitolewa bure kwa watu masikini. Mfumo wa Didier Drogba ulianzishwa mwaka 2007, kwa lengo la kusaidia matatizo ya afya na elimu Afrika.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: DROGBA ACHANGISHA PAUNI MILIONI 1.2 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top