Drogba, ataibeba Chelsea leo? |
KLABU
ya Chelsea leo itashambulia kuanzia dakika ya mwanzo katika kujaribu kumlipia
kisasi Andre Villas-Boas aliyepigwa mabao 3-1 katika mechi ya kwanza hatua ya
16 Bora Ligi ya Mabingwa Ulaya hatua ya 16 bora dhidi ya Napoli, timu ya zamani
ya Maradona.
Klab
hiyo ya London imemfukuza kocha kijana Mreno, tangu mwezi uliopita baada ya
mechi ya kwanza na sasa Mtaliano Roberto Di Matteo, amabye huu utakuwa mtihani wake
wa kwanza Ulaya unaweza kuwa mwisho iwapo wachezaji wake wasipombeba.
Chelsea
wanaweza kutinga Robo Fainali, wakipigana kama ilivyofanya klabu nyingine ya
Ligi Kuu, Arsenal ambao walishindwa kidogo walipokuwa kwenye mtihani mzito wiki
iliyopiota.
Arsenal
walifungwa 4-0 katika mechi ya kwanza na AC Milan, lakini katika marudiano
wakashinda 3-0 na kutolewa kwa jumla ya mabao 4-3.
Kwa
Chelsea, kazi ni nyepesi zaidi ya hiyo ikiwa Napoli wanasaka ushindi wa sita
mfululizo katika mashindano yote.
“Kuanzain
dakika ya kwanza tutajaribu kutengeneza nafasi za kufunga mabao. Tunatambua
wana washambuliaji wazuri na tunatakiwa kuwa makini na wao, lakini tutashambulian
kuanzia dakika ya kwanza,"alisema winga Juan Mata.
Bao
la Mata dhidi ya Napoli katika mchezo wa kwanza limepunguza kazi, kwani sasa
ushindi wa 2-0 mjini London leo utaiwezesha England angalau kuingiza timu moja
Robon Fainali katika nafasi yao pekee iliyobaki.
“Katika
soka hakuna kisichowezekana na Stamford Bridge tumekuwa tuna matokeo mazuri
katika Ligi ya Mabingwa, hivyo nafikiri tunaweza kufanya hivyo,"alisema
Mspanyola huyo.
“Mashabiki
wote watakuwa wakitushangilia sisi, ni fainali yetu, nja tunaweza kufanya hivyo."
FAIDA
MUHIMU…
Kurejea
kwa John Terry kwenye kikosi cha kwanza katika mechi ya Jumamosi ya Ligi Kuu ambayo
walishinda 1-0 dhidi ya Stoke City kunaweza kuimarisha safu yao ya ulinzi
katika mchezo wa leo wa marudiano.
Pamoja
na hayo, kwa matumaini yote, Chelsea wanatakiwa kushinda mfululizo bila kuruhusu
nyavu zao kuguswa tangu Di Matteo aanze kazi, wakikutana na timu ambayo ipo
kwenye kasi nzuri.
Napoli
wanaingia kwenye mechi ya leo wakitoka kushindaa 6-3 dhidi ya Cagliari katika
Serie A mabao yote yakifungwa na wachezaji tofauti.
Wakati
hawajawahi kushinda England, waliwahi kutoa sare ya 1-1 na Manchester City katika
hatua ya makundi msimu huu, ambayo inaweza kuwajengea kujiamini hata kama
wanaihofia Chelsea baada ya kile kilichofanywa na Arsenal dhidi ya Milan.
“Tuna
nafasi nzuri, lakini tutacheza kama mechi iko 0-0,”alisema beki Paolo Cannavaro.
Kocha
wa Napoli, Walter Mazzarri atakaa kwenye benchi leo, baada ya kiusitishwa kwa
adhabu yake kuwa nje mechi mbili.
Vikosi
vinavotarajiwa:
CHELSEA:
1-Petr
Cech; 2-Branislav Ivanovic, 24-Gary Cahill, 26-John Terry, 3-Ashley Cole;
8-Frank Lampard, 7-Ramires; 23-Daniel Sturridge, 10-Juan Mata, 5-Michael
Essien; 11-Didier Drogba
NAPOLI:
1-Morgan
De Sanctis; 14-Hugo Campagnaro, 28-Paolo Cannavaro, 6-Salvatore Aronica;
11-Christian Maggio, 23-Walter Gargano, 88-Gokhan Inler, 18-Juan Zuniga;
17-Marek Hamsik, 7-Edinson Cavani, 22-Ezequiel Lavezzi
0 comments:
Post a Comment