Karim-Benzema mazoezini jana |
MSHAMBULIAJI Karim Benzema amerejea kazini Real Madrid na
leo anatarajiwa kuwamo katika kikosi cha timu hiyo kinachoifuata Real Betis kwenye
La Liga, baada ya wiki tatu za kuwa nje kwa sababu ya maunmivu.
Mfaransa huyo hajacheza tangu atolewe nje baada ya kuumia
katika sate ya 1-1 na CSKA Moscow kwenye Ligi ya Mabingwa mechi ya kwanza ya
hatua ya 16 Bora, Februari 21, lakini anaweza kucheza kwenye mechi ya marudiano
Jumatano ijayo.
“Natumaini atakuwa tayari kucheza kesho (leo) kama haitakuwa
na athari yoyote,”alisema jana kocha Jose Mourinho katika mazoezi ya mwisho
kabla ya mechi ya leo.
"Kama kutakuwa kuna athari yoyote, hatutamchezesha wakati
tuna miezi miwili zaidi katika michuano hii."
Benzema ni mfungaji bora wa pili katika klabu hiyo baada ya
Cristiano Ronaldo, akiwa ametikisa nyavu mara 21 katika mashindano yote.
Angel Di Maria na Fabio Coentrao wapo nje kwa sababu ya
majeruhi, wakati Ricardo Carvalho anatumuikia adhabu. Real inaongoza ligi kwa
pointi zake 67 na ina mechi 13 zaidi kabla ya kumaliza ligi hiyo, ikiwazidi
pointi 10 mabingwa watetezi, Barcelona wanaoshika nafasi ya pili.
0 comments:
Post a Comment