Kikosi cha Inter kilichoaga Ulaya |
WIKI moja baada ya Lionel Messi kuibuka mchezaji wa kwanza
kufunga mabao matano kwenye Ligi ya Mabingwa, mshambuliaji wa Ujerumani, Mario
Gomez alikaribia kufuikia rekodi hiyo jana alipoiongoza Bayern Munich kutinga Robo
Fainali ya Ligi ya Mabingwa.
Gomez alikuwa mchezaji wa nane kufunga mabao manne kwenye
moja wakati mabingwa hao mara nne Ulaya wakiiadhibu FC Basel mabao 7-0 na
kulipa kisasi cha kupigwa 1-0 katika mchezo wa kwanza hivyo kufuzu kwa matokeo
ya jumla ya 7-1.
Arjen Robben pia alipiga mabao mawili kwa Bayern, ambayo
inaungana na Marseille kufuzu kwa hatua inayofuata licha ya kiufungwa na Inter Milan
2-1.
Mshabuliaji wa Inter, Diego Milito alisawazisha na jkufanya
sare ya jumla ya 1-1 hivyo mchezo kuhamia kwenye dakika za nyongeza kabla ya
kila timu kufunga na kufanya sare ya 2-2, hivyo wageni kunufaika kwa faida ya
bao la ugenini.
Marseille inaingia Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa kwa mara
ya kwanza tangu mwaka 1993.
Kipa Steve Mandanda wa Marseille aliyeokoa mabao mengi ya
wazi alitolewa nje kwa kadi nyekundu akisababisha na penalti ambayo ilitupiwa
kwenye kamba na Giampaolo Pazzini, ingawa haikuisaidia Inter kusonga mbele.
Mandanda atakosa mechi za Robo Fainali, hatua ambayo Marseille
inaweza kukutana na Messi na mabingwa watetezi, Barcelona, mabingwa mara saba AC
Milan, mabingwa mara mbili Benfica au ‘wa kuzuka’ APOEL Nicosia.
Mabingwa wa kihistroria wa michuano hiyo, (mara tisa) Real
Madrid watatafuta nafasi ya kusonga mbele kwenye Uwanja wa nyumbani kwa
kumenyana na CSKA
Pamoja na kushinda kufikia rekodi ya Messi, lakini Gomez amefikia
rekodi ya Dado Prso mwaka 2003, kufunga mabao manne ndani ya dakika 23.
0 comments:
Post a Comment