// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); BARCA NA AC MILAN, REAL MADRID NA TIMU YA KANIKI, NDIKUMANA - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE BARCA NA AC MILAN, REAL MADRID NA TIMU YA KANIKI, NDIKUMANA - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Friday, March 16, 2012

    BARCA NA AC MILAN, REAL MADRID NA TIMU YA KANIKI, NDIKUMANA


    Wachezaji wa Barcelona, bingwa mtetezi Ligi ya Mabingwa Ulaya
    MABINGWA watetezi, Barcelona wamepewa kigongo, mabingwa wa Italia, AC Milan katika droo ya Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, iliyopangwa mchana huu.
    Vibonde APOEL Nicosia ya Cyprus, timu iliyowahi kumtaka Joseph Kaniki akiwa Simba SC mwaka 2004 ambayo pia amewahi kuichezea mume wa mwigizaji Irene Uwoya, Hamadi Ndikumana ‘Katauti’ imepangwa na Real Madrid wakati Chelsea, timu pekee kutoka Ligi Kuu ya England iliyosalia kwenye michuano hii, imepangwa na mabingwa wa zamani mara mbili, Benfica ya Ureno.
    Bayern Munich ya Ujerumani, ambao Uwanja wao utapokea fainali ya michuano hii Mei 19, itamenyana na Olympique Marseille ya Ufaransa.
    "Ni vuzuri tunaanzia ugenini na tunaweza kujenga msingi kutoka hapo," alisema Ofisa Mtendaji Mkuu wa Chelsea, Ron Gourlay, ambaye timu yake imeitoa Napoli kwa mbinde.
    "Ramires na David Luiz watajua zaidi kuhusu Benfica na pia tunajua zaidi kuhusu Benfica, kwa sababu waliongoza kundi ambalo lilikuwa Manchester United na timu ni nzuri."
    Kocha Msaidizi wa Marseille, Guy Stephan, ambaye timu yake iliitoa kwa mbinde Inter Milan katika 16, Bora aliiambia L'Equipe TV: "Itakuwa mechi muhimu sana ambayo itakuja mwishoni mwa msimu wetu. Tutakuwa na wakati mgumu kuanzia nyumbani.
    "Lakini tuna rekodi nzuri, tayari tumeifunga timu ya Ujerumani msimu huu. Na Borussia Dortmund inaongoza Bundesliga mbele ya Bayern. Pia tulifanya vitu dhidi ya Inter ambayo tulipata nafasi nyingi dakika za mwishoni."
    Barca na Milan tayari zimekutana katika hatua ya makundi msimu huu na matokeo yalikuwa sare ya 2-2 kwenye Uwanja wa Nou Camp kabla ya ushindi wa 3-2 kwa Barca kwenye Uwanja wa San Siro wakati timu zote zikiwa zimekwishafuzu hatua ya mtoano.
    Katika Nusu Fainali, Milan au Barcelona timu mojawapi itamenyana na mshindi kati ya Benfica na Chelsea. Mshindi wa mechi kati ya Bayern na Marseille atamenyana na Real au APOEL.
    Fainali kati ya Real na Barca ni jambo ambalo linatarajiwa sana. Tena sana.
    Mechi za kwanza za Robo Fainali zitachezwa Machi 27 na 28 na marudiano Aprili 3 na 4. Mechi za kwanza za Nusu Fainali zitachezwa April 17 na 18 na marudiano Aprili 24 na 25.

    RATIBA ROBO FAINALI:
    Apoel Nicosia v Real Madrid
    Olympique Marseille v Bayern Munich
    Benfica v Chelsea
    AC Milan v Barcelona

    NUSU FAINALI:
    Olympique Marseille/Bayern Munich v APOEL Nicosia/Real Madrid
    Benfica/Chelsea v AC Milan/Barcelona
    (Mechi za kwanza robo fainali zitachezwa Machi 27 na 28, marudiano Aprili 3 na 4, wakati nusu fainali za kwanza zitakuwa Aprili 17 na 18 na marudiano Aprili 24 na 25- na fainali itakuwa mjini Munich, Mei 19)
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: BARCA NA AC MILAN, REAL MADRID NA TIMU YA KANIKI, NDIKUMANA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top