Charz Stunner, Gigga Flo, Ric Boi, Cyrill aka Kid, Pancho Latino Mafia, Jux Vuitton, Nas 3 |
STUDIO za B'Hits zimeibuka na mzigo mpya na wa kwanza mwaka
huu, uitwao SIRUDI TENA wa msanii Mabeste aliyemshirikisha Jux, ambaye kwa mara
ya kwanza atasikika akichana fastan fasta.
Kama kawa Pancho Latino amesimama kwenye Piano na kuifanya
track hiyo ya Mabeste iwe kali kinoma.
Pamoja na Mabeste kuimba mwenyewe, pia ndiye ameandika wimbo
huo ambao kazi nzima ya kuutayarisha imefanywa na Pancho Latino na Mixing na
Master imefanywa na Hermy B katika studio za B’Hits Studio 4, Dar es Salaam.
Habari hizi zimeshushwa kwetu bongostaz kutoka kwa Joachim
Lyimo ‘Hermy B’ ambaye ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa B Hitz Music Group Ltd.
0 comments:
Post a Comment