// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); AZAM YAPANDA KILELENI LIGI KUU - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE AZAM YAPANDA KILELENI LIGI KUU - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Saturday, March 10, 2012

    AZAM YAPANDA KILELENI LIGI KUU


    Mashabiki wa Azam wakifurahia ushindi wa leo

    AZAM imepanda kileleni mwa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara baada ya kutimiza pointi 41, kufuatia ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Yanga iliyokuwa na wahezaji tisa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam jioni hii.
    Mabao ya Azam ambayo hata hivyo imecheza mechi mbili zaidi dhidi ya Simba inayoshika nafasi ya pili kwa pointi zake 40 na Yanga ya tatu yenye pointi 40 pia, yalitiwa nyavuni na kinara wa mabao Ligi Kuu John Raphael Bocco ‘Adebayor’ dakika ya nne na 82 na lingine Kipre Balou kutoka Ivory Coast dakika ya 55.
    Bao la kufutia machozi la Yanga lilifungwa na Mwanasoka Bora wa Uganda, Hamisi Kiiza dakika ya 32.
    Katika mechi hiyo iliyotawalia na ubabe baina ya wachezaji wa timu hiyo, Yanga ilipatra hasara ya kupoteza wachezaji wawili, beki Nadir Haroub ‘Cannavaro’ dakika ya 16 tu na kiungo wa Rwanda, Haruna Niyonzima dakika ya 13.
    Cannavaro alipewa kadi nyekundu ya moja kwa moja na Niyonzima alipewa kadi ya pili za njano.
    Katika mchezo huo, kikosi cha Yanga kilikuwa; Shaaban Kado, Shadrack Nsajigwa, Stefano Mwasyika, Athumani Iddi ‘Chuji’, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Nurdin Bakari, Omega Seme, Haruna Niyonzima, Hamisi Kiiza na Shamte Ally.
    Azam: Mwadini Ally, Erasto Nyoni, Waziri Salum, Aggrey Morris, Said Mourad, Bolou Kipre, Kipre Tchetche, Ibrahim Mwaipopo/Abdi Kassim 'Babbi' dk 46, John Bocco, Salum Abubakar/Abdulhalim Humud dk 84 na Mrisho Ngassa.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: AZAM YAPANDA KILELENI LIGI KUU Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top