Kiungo Mholanzi wa AC Milan, Mark Van Bommel (kulia) akiteta na Mholanzi mwenzake, anayechezea Arsenal, mshambuliaji Robin Van Persie baada ya mechi la jana. |
Mabingwa wa Serie A waliduwazwa kipindi cha kwanza na mabao ya Laurent Koscielny, Tomas Rosicky na Robin van Persie aliyefunga kwa penalti.
Milan, ambao wametwaa taji hilo mara saba, walizinduka kipindi cha pili na kuwabana wenyeji hadi kuvuna tiketi hiyo ya kuvuka hatua hiyo ya 16 bora, lakini mashabiki wake walikuwa wana hofu ya kufa katika hatua kama hii kwenye mechi ya marudiano na Deportivo Coruna mwaka 2004.
Katika mchezo huo, Van Persie alipoteza nafasi ya wazi mno ya kufunga bao la kufanya matokeo yawe 4-4.
0 comments:
Post a Comment