MABINGWA wa Ligi Kuu ya Kenya, Tusker wametolewa katika Ligi
ya Mabingwa baada ya kufungwa 1-0 na APR mjini Kigali, Rwanda.
Nyota wa Burundi, Papy Faty alipiga bao hilo pekee dakika ya
62 na kuzima ndoto za Tusker kusonga mbele.
Mechi ya kwanza iliyochezwa Nairobi wiki mbili zilizopita
iliisha kwa sare, kocha Mholanzi wa APR, Ernie Brandts amefurahia ushindi huo.
Ilikuwa ni wiki ngumu kwa Wakenya, kwani hata Gor Mahia imetupwa
nje ya michuano ya Kombe la Shirikisho na Ferroviario De Maputo kwa jumla ya
mabao 3-0.
Tusker ilitarajiwa kurejea Nairobi jana kuendelea na kampeni
za kutetea KPL.
Gor Mahia hivi sasa inataka kumfukuza kocha wake Mcameroon
Anaba Awono kutokana na kiwango kibovu kinachoonyeshwa na timu hiyo na matokeo
mabaya kwa ujumla.
0 comments:
Post a Comment