// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); ANELKA APIGA BAO, LAKINI WACHINA WAMBEZA - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE ANELKA APIGA BAO, LAKINI WACHINA WAMBEZA - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Saturday, March 17, 2012

    ANELKA APIGA BAO, LAKINI WACHINA WAMBEZA


    Anelka
    MSHAMBULIAJI wa Kifaransa, Nicolas Anelka alipiga bao katika mechi ya kwanza ya Ligi Kuu ya Cbhina akiicheza timu yake mpya, Shanghai Shenhua japokuwa ilifungwa mabao 3-2 na wapinzani wao wakubwa, Beijing Guoan.
    Mshambuliaji huyo wa zamani wa Arsenal na Chelsea, aliisawazishia timu yake mpya, Shenhua na kupata sare ya 2-2 katika mechi ya wapinzani wa jadi wa China.
    Timu ya Anelka ilikuwa imekwishaloa 2-0, shukrani kwao Piao Cheng na kiungo Mreno, Manu.
    Mshambuliaji wa Australia, Joel Griffiths alianza kuisawazishia Shenhua, akiichezea mechi ya kwanza tangu ajiunge nayo kutoka Guoan Januari, akifunga kwa penalti na kufanya 2-1.
    Winga wa zamani wa Shanghai, Mao Jianqing alizima matumaini ya timu yake ya zamani, akiifungia Beijing bao la ushindi dakika za lala salama, katika mechi yake ya kwanza Guoan.
    Jumamosi iliyopita, Anelka aliwaangusha mashabiki baadaya kukosekana uwanjani katika mechi ya kwanza ya Shenhua katika Ligi Kuu ya China dhidi ya Jiangsu Sainty, kutokana na kuwa majeruhi.
    Mfaransa huyo alikuwa gumzo kuelekea mchezo huo kwenye Uwanja wenye uwezo wa kumeza mashabiki 68 000, Uwanja wa Workers mjini Beijing, lakini ilielezwea hakuwa fiti kiasi cha kutosha kucheza mechi hiyo.
    Aliwasalimia mashabiki 150 waliokuwa Uwanja wa ugenini ambao walijibu kwa furaha huku wakitaja jina la shujaa wao huyo mpya.
    Baadhi ya mashabiki wa Shenhua wamesafiri kwa saa 15  kwenda kuishangilia timu yao.
    "Nataka kusema, Nimekuja hapa kuisapoti timu na si Anelka", alisema shabiki wa Shanghai, David Xie, "Lakini sina matumaini na timu, hata kama amefunga bao lake la kwanza wakati timu yetu imepoteza mchezo."
    Anelka amekuwa mchezaji babu kubwa zaidi kuwahi kusajiliwa katika historia ya ligi ya China baada ya kukubali kutua Shenhua, Desemba mwaka jana kwa mshahara wa Euro 270 000 kwa wiki.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: ANELKA APIGA BAO, LAKINI WACHINA WAMBEZA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top