// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); AZAM FC YAICHIMBIA KABURI KENGOLD, YAICHAPA 2-0 SOKOINE - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE AZAM FC YAICHIMBIA KABURI KENGOLD, YAICHAPA 2-0 SOKOINE - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
    Thursday, April 03, 2025

    AZAM FC YAICHIMBIA KABURI KENGOLD, YAICHAPA 2-0 SOKOINE


    TIMU ya Azam FC imeibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya wenyeji, Kengold katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara leo Uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya.
    Mabao ya Azam FC yamefungwa na winga Mgambia, Gibrill Sillah dakika ya 28 na kiungo mshambuliaji, Nassor Saadun Hamoud dakika ya 40.
    Kwa ushindi huo, Azam FC inafikisha pointi 51, ingawa inabaki nafasi ya tatu ikizidiwa pointi sita na Simba SC ambayo pia ina mechi mbili mkononi na wote wapo nyuma ya mabingwa watetezi, Yanga wenye pointi 61 za mechi 23.
    Kwa upande wao Kengold baada ya kupoteza mchezo huo wanabaki na pointi zao 16 baada ya kucheza mechi 24 na wanaendelea kushika mkia kwenye ligi ya timu 16.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: AZAM FC YAICHIMBIA KABURI KENGOLD, YAICHAPA 2-0 SOKOINE Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry