// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); TAIFA STARS YACHAPWA 2-0 NA MOROCCO KIFUZU KOMBE LA DUNIA - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE TAIFA STARS YACHAPWA 2-0 NA MOROCCO KIFUZU KOMBE LA DUNIA - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
    Wednesday, March 26, 2025

    TAIFA STARS YACHAPWA 2-0 NA MOROCCO KIFUZU KOMBE LA DUNIA


    TIMU ya taifa ya soka ya Tanzania usiku wa kuamkia leo imechapwa mabao 2-0 na wenyeji, Morocco katika mchezo wa Kundi E kufuzu Fainali za Kombe la Dunia 2026 zinazoandaliwa kwa pamoja na Marekani, Canada na Mexico.
    Mabao ya Simba wa Atlasi yaliyoizamisha Taifa Stars yamefumgwa na beki wa Real Sociedad, Nayef Aguerd dakika ya 51' na kiungo wa Real Madrid, Brahim Díaz kwa Penalti dakika ya 58 Uwanja wa Halmashauri ya Mji wa Oujda.
    Kwa matokeo hayo, Morocco inafikisha pointi 15 katika mchezo wa tano, ikiendelea kuongoza Kundi E, wakati Tanzania inabaki nafasi ya tatu kwa pointi zake sita ikizidiwa tu wastani wa mabao na Niger baada ya wote kucheza mechi nne.
    Timu nyingine kwenye Kundi hilo, Zambia inashika mkia kwa pointi zake Tatu za mechi nne pia.
    Timu nyingine mbili zilizopangwa katika Kundi hilo, Eritrea ilijitoa na Kongo - Brazzaville imeenguliwa baada ya kufungiwa na Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) ikiwa tayari imecheza mechi tatu na kufungwa zote.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: TAIFA STARS YACHAPWA 2-0 NA MOROCCO KIFUZU KOMBE LA DUNIA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry