// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); NAMUNGO FC YAZINDUKA NA KUICHAPA COASTAL UNION 2-0 CHAMAZI - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE NAMUNGO FC YAZINDUKA NA KUICHAPA COASTAL UNION 2-0 CHAMAZI - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Tuesday, September 17, 2024

    NAMUNGO FC YAZINDUKA NA KUICHAPA COASTAL UNION 2-0 CHAMAZI


    TIMU ya Namungo FC imepata ushindi wa kwanza katika Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara baada ya kuichapa Coastal Union mabao 2-0 jioni ya leo Uwanja wa Azam Complex, Chamazi Jijini Dar es Salaam.
    Mabao ya Namungo FC yamefungwa na Ritch Nkoli dakika ya 38 na Pius Buswita dakika ya 45’+2 huo ukiwa ushindi wa kwanza timu hiyo ikitoka kupoteza mechi tatu mfululizo kwa kufungwa 2-1 na Tabora United, 2-0 na Fountain Gate na 1-0 na Dodoma Jiji .
    Kwa upande wao Coastal Union wanafikisha mechi tatu bila ushindi, kufuatia awali kutoa sare na KMC 1-1 , kabla ya kufungwa 1-0 na Mshujaa zote Uwanja wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni (KMC Complex), Mwenge Jijini Dar es Salaam.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: NAMUNGO FC YAZINDUKA NA KUICHAPA COASTAL UNION 2-0 CHAMAZI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top