UJERUMANI imepanda kileleni mwa Kundi D katika mbio za Euro 2016 kufuatia ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Poland mjini Frankfurt.
Thomas Muller na Mario Gotze wote walifunga mabao yaliyoifanya Ujerumani iongoze 2-0 hadi mapumziko, lakini Robert Lewandowski akaifungia Poland moja.
Gotze akafunga bao lake la pili katika mchezo na la tatu kwa Ujerumani dakika za lala salama ikiibuka na ushindi wa 3-1.
Kikosi cha Ujerumani kilikuwa; Neuer, Can, Boateng, Hummels, Hector, Schweinsteiger, Kroos, Muller, Ozil, Bellarabi/Gundogan dk53 na Gotze/Podolski dk90.
Poland; Fabianski, Piszczek/Olkowski dk43, Szukala, Glik, Rybus, Grosicki/Peszko dk86, Jodlowiec, Krychowiak, Milik, Lewandowski, Maczynski/Blaszczykowski dk63.
Mshambuliaji wa Bayern Munich, Mario Gotze akishangilia baada ya kuifungia Ujerumani bao la pili PICHA ZAIDI GONGA HAPA
0 comments:
Post a Comment